Ninayo furaha ya kukukaribisha katika tovuti ya Mamlaka ya Serikali Mtandao, tunatuamaini utapata habari zenye kuaminika na zilizo kamili zitakazokupa muongozo kuhusu dira, muelekeo, malengo mikakati, shughuli kuu pamoja na maadili ya Mamlaka.
Lengo kuu la tovuti hii ni kufikia miongoni mwa matarajio ya Mamlaka ya kuendeleza na kurahisisha matumizi ya Tehama ndani ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na kuboresha mfumo wa utoaji wa huduma katika wizara, idara na taasisi mbali mbali za serikali kwa ajili ya wananchi. Matumizi ya TEHAMA hutoa matokeo mazuri kutokana na kuboresha utoaji huduma kwa watumishi wa umma na wananchi kwa jumla kwa kutumia miundombinu ya TEHAMA inayosimamiwa kwa weledi ili kuindeleza na kuikuza Zanzibar kiuchumi.
Tovuti hii inatarajia kuendelea kutoa taarifa mbali mbali kuhusiana na hatua madhubuti pamoja mikakati imara inayochukuliwa na Serikali kupitia Mamlaka ya Serikali Mtandao katika utekelezaji wa majukumu yake ili kutimiza malengo ya Mamlaka kama yalivyoelezwa katika mipango mkakati na sera ya Serikali Mtandao
Ni matumaini yangu kuwa tovuti hii itatoa habari bora zaidi, zilizo sahihi na kwa wakati unaofaa ili kuwezesha upatikanaji wa habari na huduma kwa watanzania wote na wageni wa ndani na nje.
Mwisho, natoa wito kwa wadau wote kuendelea kuperuzi tovuti yetu mara kwa mara na kuwasihi kuwasiliana nasi kwa maoni, ushauri kwa ajili ya uboreshaji au kuhitaji ufafanuzi zaidi juu ya huduma zetu
Shukrani
Mamlaka ya Serikali Mtandao
Zanzibar