Ofisi ya Rais- Ikulu

MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO ZANZIBAR

Majukumu ya Mamlaka

Kwa mujibu wa Sheria Na. 1 ya Mwaka 2024, majukumu ya eGAZ ni pamoja na:

  1. Kuratibu utekelezaji wa Serikali Mtandao Zanzibar, ikiwa ni pamoja na uundaji wa sera, viwango, na miongozo ya TEHAMA serikalini.
  2. Kusimamia na kuendeleza miundombinu ya TEHAMA ya Serikali, kama vile Data Center, Mtandao wa Serikali, huduma za usalama mtandao, nk.
  3. Kutoa huduma za pamoja (shared services) kwa taasisi za serikali kama mfumo wa barua pepe rasmi, mifumo ya malipo, hifadhi ya taarifa, nk.
  4. Kuhakikisha usalama wa taarifa za serikali kwa njia ya kidijitali, kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama wa kimtandao.
  5. Kutoa mafunzo, ushauri wa kitaalamu na kujenga uwezo kwa taasisi za serikali kuhusu matumizi sahihi ya TEHAMA.
  6. Kufanya tafiti, tathmini na kutoa mapendekezo ya kisera na kiufundi kuhusu matumizi ya teknolojia katika sekta ya umma.
  7. Kuhamasisha matumizi ya TEHAMA kwa wananchi, ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za serikali kwa njia ya mtandao.
  8. Kusimamia maendeleo ya mifumo ya kitaifa ya TEHAMA, kama mifumo ya usajili, malipo, afya, elimu, biashara, utalii, nk.
  9. Kuratibu ushirikiano wa kimataifa na mashirika ya maendeleo katika nyanja za TEHAMA na Serikali Mtandao.