Ofisi ya Rais- Ikulu

MAMLAKA YA SERIKALI MTANDAO ZANZIBAR

Muundo wa Mamlaka

Mamlaka ya Serikali Mtandao Zanzibar (eGAZ) imeundwa kwa mujibu wa Sheria ya Mamlaka ya Serikali Mtandao Zanzibar Na. 1 ya Mwaka 2024, ikiwa taasisi huru ya umma chini ya Ofisi ya Rais, inayosimamia masuala ya TEHAMA na Serikali Mtandao.

Muundo wa eGAZ unajumuisha vitengo na idara kuu zifuatazo:

  1. Bodi ya Wakurugenzi
    • Chombo cha juu cha kutoa mwelekeo wa kimkakati na kusimamia utendaji wa Mamlaka.
    • Inahakikisha uwajibikaji, uwazi na ufanisi wa eGAZ.
  2. Mkurugenzi Mkuu
    • Mtendaji Mkuu wa Mamlaka, anayeongoza shughuli za kila siku.
    • Anawajibika kwa utekelezaji wa sera, mipango, na mikakati ya eGAZ.
  3. Idara Kuu za Mamlaka ya Serikali Mtandao
    1. Idara ya Usimamizi wa Miundombinu na Mifumo ya TEHAMA
      • Kusimamia na kuendeleza miundombinu ya TEHAMA ya Serikali pamoja (mitandao, vituo vya data, n.k).
      • Kuhakikisha usalama na uimara wa huduma za kidijitali.
      • Kuratibu na kusimamia maendeleo, utekelezaji na uunganishaji wa mifumo ya Serikali Mtandao.
    2. Idara ya Huduma za TEHAMA kwa Taasisi za Serikali
      • Kutoa huduma za ushauri wa kitaalamu wa TEHAMA kwa taasisi za serikali.
      • Kur atibu uunganishaji wa huduma za TEHAMA serikalini.
      • Kutoa miongozo ya viwango na usalama wa mifumo.
      • Kuandaa sera, mikakati, miongozo na tafiti kuhusu matumizi ya TEHAMA katika sekta ya umma.
      • Kufanya tathmini na ufuatiliaji wa utekelezaji wa programu za TEHAMA.
    3. Idara ya Utumishi, Mipango na Rasilimali
      • Kusimamia rasilimali watu, fedha, manunuzi, na huduma nyingine za kiutawala.