Ujumbe wa Mkurugenzi

Ninayo furaha ya kukukaribisha katika tovuti ya wakala wa serikali mtandao, tunatuamaini utapata habari zenye kuaminika na zilizo kamili zitakazokupa muongozo kuhusu dira, muelekeo, malengo mikakati, shughuli kuu pamoja na maadili ya wakala.

Lengo kuu la tovuti hii ni kufikia miongoni mwa matarajio ya wakala ya kuendeleza na kurahisisha matumizi ya Tehama ndani ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na kuboresha mfumo wa utoaji wa huduma katika wizara, idara na taasisi mbali mbali za serikali kwa ajili ya wananchi. Matumizi ya TEHAMA hutoa matokeo mazuri kutokana na kuboresha utoaji huduma kwa watumishi wa umma na wananchi kwa jumla kwa kutumia miundombinu ya TEHAMA inayosimamiwa kwa weledi ili kuindeleza na kuikuza Zanzibar kiuchumi.

Tovuti hii inatarajia kuendelea kutoa taarifa mbali mbali kuhusiana na hatua madhubuti pamoja  mikakati imara inayochukuliwa na  Serikali kupitia Wakala wa Serikali Mtandao katika utekelezaji wa majukumu yake ili kutimiza malengo ya wakala kama yalivyoelezwa katika mipango mkakati na sera ya Serikali Mtandao

Ni matumaini yangu kuwa tovuti hii itatoa habari bora zaidi, zilizo sahihi na kwa wakati unaofaa ili kuwezesha upatikanaji wa habari na huduma kwa watanzania wote na wageni wa ndani na nje.

Mwisho, natoa wito kwa wadau wote kuendelea kuperuzi tovuti yetu mara kwa mara na kuwasihi kuwasiliana nasi kwa maoni, ushauri kwa ajili ya uboreshaji au kuhitaji ufafanuzi zaidi juu ya huduma zetu

Shukrani

Wakala wa Serikali Mtandao

Zanzibar