Maswali

Ni mabadiliko ya utoaji huduma za Serikali kwa ufanisi,urahisi na uwazi kwa raia /wananchi na wafanyabiashara kwa kutumia TEknolojia ya HAbari na MAwasiliano (TEHAMA)

 

  • Kuwa na viwango bora vya utoaji huduma,
  • Kusogeza taarifa na huduma kwa wananchi,
  • Kuongeza ufanisi wa utoaji huduma,
  • Kuengeza uwazi na uwajibikaji ,
  • Kushirikisha wananchi katika maamuzi pamoja na
  • Kudhibiti udanganyifu na rushwa
  1. Huduma za Ushauri wa Kitaalamu na Msaada wa Kiufundi
  2. Barua pepe za Serikali
  3. Huduma ya Kuhifadhi Mifumo na tovuti
  4. Huduma za mtandao Serikalini
  5. Utengenezaji wa Mifumo shirikishi

Wakala wa Mkonga na miundombinu ya TEHAMA ni taasisi inayosimamia na kusambaza miundombinu ya TEHAMA serikalini pamoja na kusimamia  kituo kikuu cha kuhifadhia taarifa (Data Center).

Wakala wa Serikali Mtandao ni taasisi inayosimamia Huduma za TEHAMA serikalini ikiwemo kutoa miongozo, sera na kanuni, utengenezaji wa mifumo , usimamizi wa miradi, ununuzi wa vifaa, huduma za kimtandao pamoja na kutoa ushauri wa kitaalamu juu ya matumizi ya TEHAMA.

Barua pepe ya Serikali ni barua pepe maalumu inayotengenezwa kwa anuani maalum za Serikali kwa ajili ya kusaidia mawasiliano ya kikazi ya kila siku kwa watumishi wa Umma.

Kupata barua pepe ya Serikali, Mtumishi anatakiwa kuandika barua kwa Wakala wa Serikali Mtandao kuomba kutengenezewa barua pepe na hatua nyengine zitafuata.

Nyaraka za mifumo zilizomo ndani ya tovuti zitatumika kulingana na mahitaji.

  1. Ukitaka kuanzisha mfumo mpya, pakua nyaraka ya Dhana ya Uanzishaji wa Mfumo/Mradi.
  2. Kwa mfumo ambao umeshaanza na unaendelea, pakua nyaraka ya Ripoti ya Utekelezaji wa Mfumo/Mradi
  3. Kwa mfumo ambao umeshakamilika, pakua nyaraka ya Ripoti ya Kukamilisha Mfumo/Mradi
  4. Kwa kuwasilisha mahitaji ya mfumo kwa msimamizi (Consultant) au Mtengenezaji, pakua nyaraka ya Hadidu Rejea ya Mfumo/Mradi

Nyaraka zote zinatakiwa zijazwe kulingana na maelezo yaliyomo, zisainiwe na wahusika na ziwasilishwe Wakala wa Serikali Mtandao kwa ajili ya kuidhinishwa.Ili kupata nyaraka hizi bonyeza anuani hii Mwanzo/Nyaraka.